Wednesday, September 22

SHALOM

Shalom mwana wa Mungu aliye hai.

Yohana 14:27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.
Neno Shalom (שלום) maana yake ni AMANI.
Shalom (AMANI) ni salamu ya jadi ya Kiebrania, lakini Shalom (AMANI) ya Yesu ni zawadi ya wokovu, ikimaanisha neema/fadhila za baraka za Kimasihi.
Shalom (AMANI) kama salamu ya jadi ya Kiebrania, Yesu katika mwili aliikuta na angeweza kabisa kutuachia hii Shalom ya Kiebrania kama salamu, lakini Yesu hakutuachia wala hakutupa Shalom (AMANI) ya salamu ya jadi ya Kiebrania bali alituachia na kutupa Shalom (AMANI) yake mwenyewe ambayo ni zawadi ya wokovu ikiwa na maana neema au fadhila za baraka za Kimasihi.
Yaani Yesu anatuambia hatoi AMANI kama ulimwengu utoavyo, najua ulishawahi kutana na watu wengi anasema ngoja niende ufukweni, mahali pa utulivu nisikilize na kimziki fulani kilaini hivi nirejeshe AMANI baada ya msongo wa wiki nzima kazini, kwenye biashara au kilimo, ndiyo wanakwenda na wanapata amani lakini baada ya muda akikumbana na changamoto za kimaisha ile AMANI inapotea, kwa hiyo inabidi atafute njia nyingine kuirejesha AMANI tena.
AMANI ya Yesu aliyotuachia na kutupa kamwe haipotei kwa sababu AMANI ya Yesu ni Yesu mwenyewe kwani neno la Mungu linatuambia Yesu ni Mfalme wa AMANI.
Isaya 9:6 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.
Hii AMANI ya Yesu ipo ndani yako kwa sababu Yeye na Baba yake wanafanya makao ndani yako kwa sababu umempenda Yesu na kulishika neno lake.
Yohana 14:23 Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
Kama hujampenda Yesu na kulishika neno lake nakushauri ufanye hivyo sasa, bofya kiungo hapo chini upate maelekezo ya kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako ili umpokee Roho Mtakatifu naye atakumiminia pendo la Mungu ndani yako ili uweze kumpenda Yesu. Kuna wengine inawezekana walikuwa wanasema tunampenda Yesu lakini ukweli ni kwamba huwezi mpenda Yesu pasipo kuwa na pendo la Mungu ndani yako ambalo linamiminwa na Roho Mtakatifu kwenye moyo wako.
Warumi 5:5 na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.
Huyu Shalom ndiye alikuwa na akina Shedraki, Meshaki na ABednego kwenye tundu la simba, anapokuwa ndani yako AMANI yako ni ya kudumu
Daniel 3:25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.
Nimekusalimu kwa salamu ya Kimasihi, na sio ile Shalom ya jadi ya Kiebrania.
Shalom, Shalom.



No comments:

Post a Comment

Barikiwa kwa ujumbe wako.