Maana Neno la Mungu
li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili,
tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani
yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Waebrania
4:12. Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe, Yeye ndiye msaada uliopo wakati wa
taabu. Wakati tunapitia kwenye majaribu na mateso katika maisha yetu, omba NENO
na maadui watakukimbia. Maadui wanamwogopa Mungu na neno lake, kwa sababu li hai, tena lina nguvu, na hata linadhuru na ni
hatari. Hapa kuna baadhi ya maandiko ya maombi, ili kukusaidia maisha yako ya
maombi, na kupata nguvu za kiroho katika kipindi cha udhaifu.
OMBA
MAOMBI HAYA KILA SIKU ASUBUHI, MCHANA NA USIKU.
Baba
umenipa funguo muhimu katika Mathayo 16:19 za kufunga na kufungua. Ninatumia
funguo hizo kufunga na kufungua, kuvunja na kubamiza kila kitu ambacho kinazuia
kutimizwa kwa mipango yako kamili katika maisha yangu. Ninaamuru na kutangaza
kwamba kila mnyororo, kamba, gereza, pingu kwamba zimefunguliwa, zimekatwa, na
kuondolewa kutoka kwenye maisha yangu katika jina la Yesu.
Baba, Bwana Nakushukuru, kwamba
wewe pekee ndiye hakimu wa maisha yetu, kwa mujibu wa Yeremia 17:9-10 Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa
kufisha; nani awezaye kuujua? Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno,
hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.
Baba
naomba katika jina la Yesu, kwa mujibu wa Zaburi 22:19 Nawe,
Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. Baba naomba
kwamba utusaidie, na kutupa uvumilivu wa
kusubiri mapenzi yako kutimizwa.
Baba katika jina la Yesu, neno lako liniasema
katika Isa 41:10-12 usiogope, kwa maana mimi ni
pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam,
nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote
walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe
watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe;
watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu
yako.
Baba,
ninakubaliana na neno lako lenye nguvu, uweza, uhakika, na la kujiamini, kwamba
utawalinda watu wako dhidi ya maadui. Umetuambia kwamba kisasi ni chako asema
Bwana, na utawalipa waovu. Bwana Ninakushukuru, kwa ajili ya ulinzi wako, na
neno lako la nguvu na la ukombozi. Katika jina la Yesu.
Baba
tunakushukuru kwa neno lako linalosema katika Ayubu 5:12 Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu, Mikono yao
isipate kuyatimiza makusudi yao. Baba wa Mbinguni, ninachukua mamlaka ya
neno lako kufunga, kufuta na kung’oa mipango yote miovu ya adui, nakuifanya
kuwa utupu, batili, na kuifuta kwa jina la Yesu.
Baba katika jina la Yesu, umesema
katika Zaburi 27:2 "Watenda mabaya
waliponikaribia, wanile nyama yangu, watesi wangu na adui zangu, walijikwaa
wakaanguka." Asante Bwana kwa ulinzi wako. Asante Bwana, kwasababu
unatalnda. Wakati maadui zetu wanakuja
kula nyama yetu, tunakuwa dhaifu, tumelala kiroho, tumekata tamaa, lakini uwezo wako katika damu umeruhusu
maadui kuanguka ndani ya shimo la kuzimu. Asante Mungu wa huruma na neema, kwa
upendo wako wa milele kwa watu wako.
Baba
neno lako linasema nami katika Luka 10:19 kwamba “Tazama,
nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala
hakuna kitu kitakachowadhuru.” Bwana natumia uwezo wako na mamlaka yako,
ili kuvunja, kubamiza, kuponda, kung’oa, kutawanya vipande vipande, kila
mipango ambayo shetani ameandaa dhidi ya maisha yangu, familia yangu, huduma
yangu, nyumba yangu, uhusiano, fedha, na vitu vyote vilivyo vyangu. Nakushukuru
Bwana, na ninadai ushindi kamili katika jina la Yesu.
Baba nasimama sawa sawa na neno
lako katika Ayubu 6: 8 linalosema “Laiti ningepewa haja yangu, Naye Mungu angenipa neno hilo
ninalolitamani sana!” Bwana Naomba katika jina la Yesu kwamba ombi letu utalijibu
kulingana na mapenzi yako na kwa wakati, na utatupa vitu vilivyomo katika
mapenzi yako kwa ajili yetu.
Baba katika jina la Yesu kulingana
na Wafilipi 4:6 unatuambia “Msijisumbue kwa neno lo
lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja
zenu na zijulikane na Mungu.” Bwana nakushukuru, kwamba tunaweza kuja
kwako wakati wowote kwa maombi ili haja zetu zijulikane kwako.
Baba
kama ulivyosema katika Zaburi 23:1 Wewe ni mchungaji wangu, sitapungukiwa au kukosa
vitu vyovyote vizuri katika maisha yangu. Wewe ni Mungu ambaye unatupatia
mahitaji yetu yote. Nakiri kama ulivyosema, kwamba huwezi kuzuia mambo yoyote
mazuri kwa watoto wako. Baba nadai faida zako zote za kiroho, na za kimwili.
Katika Jina la Yesu.
Baba
umetuambia katika neno lako, katika Luka 17:6 kwamba “Bwana
akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu
huu, Ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.” Baba nachukua mamlaka
ya neno lako leo, na kung’oa madeni yote ya kifedha, kila mapambano, kila
misiba, kila ukosefu, uhitaji, na roho zote zinazoshambulia fedha zetu, afya,
ndoa, nyumba, watoto, huduma, kazi zetu, na yote yaliyo yetu. Nazifunga, nakuzing’oa toka kwenye maisha yetu, na kuzitupa katika
bahari. Katika jina la Yesu.
Baba umeniambia katika 2 Tim.
4:18 kwamba “Bwana ataniokoa na kila neno baya, na
kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na
milele. Amina.” Baba nakushukuru kwa kuwa umeniokoa na kila matendo
maovu ya adui, na kunihifadhi kwa ajili ya ufalme wako wa mbinguni. Baba
ninasimama sawa sawa na neno lako na kuyafunga kila matendo maovu, yaliyofanywa
maishani kwangu, watoto wangu, familia yangu, nyumbani kwangu, huduma yangu,
afya yangu, fedha zangu, mustakabali wangu na vitu vyote tunavyomiliki. Ninayafunga
toka mashariki, magharibi, kaskazini na kusini, mbingu ya pili, katika maji, kwenye
moto, katika hewa, katika ardhi, katika maeneo, katika mazingira, na kila
maeneo chini ya jua, mwezi, nyota, na sehemu nyingine zote za siri yanakojificha.
Ninaachilia neno lako, damu ya Yesu, na jina lako dhidi yao, katika maeneo hayo
yote, kwamba yatakuwa yamefungwa milele na milele amina.
Baba natumia funguo muhimu katika
Mathayo 18:18 kwamba “na yo yote mtakayoyafungua
duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.” Ninajifungua, pamoja na kila
kitu changu, toka kila mnyororo, vifungo, pingu, na kamba katika jina la Yesu.
Baba
kama ulivyosema katika kitabu cha Hesabu 11:1. Nasimama kwenye mamlaka ya neno
lako, na amrisha moto ushuke kutoka mbinguni na kuharibu kila roho ya kurudi
nyuma ambayo imewekwa na adui katika maisha yetu. Katika jina la Yesu.
Baba,
Bwana nasimama sawasawa na neno lako katika Joshua 1:8. Naomba maneno yako
yasindoke vinywani mwetu wala mioyoni mwetu, bali tuyatafakari mchana na usiku,
ndipo tutakapoifanikisha njia yetu.
Bwana
ninaomba mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote
yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye
kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri
yo yote, niyatafakari hayo sawasawa na neno lako, katika Wafilipi 4: 8.
Baba umeniambia katika 2 Timotheo
1:7 kwamba Mungu hakunipa roho ya woga, bali ya nguvu
na ya upendo na ya moyo wa kiasi. Baba napinga roho ya woga, nakataa
kuwa na wasiwasi, au kukatishwa tamaa. Nautumia nguvu yako na mamlaka juu ya
kila mipango na miradi ya adui. Nadai ushindi
kamili juu ya nguvu zote za giza, katika jina la Yesu.
Baba neno lako linasema katika
Yer 23:29 " Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo
mawe vipande vipande? Baba katika jina la Yesu, natumia moto wa Mungu kuteketeza kila uovu
dhidi yangu, na wapendwa wangu, toka mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
Natumia nyundo ya neno la Mungu kuvunja kila uovu wa vifungo vya nafsi,
uhusiano wa damu, uchawi na laana zote mababu, uliopitia kwa uzao wetu. Najifunika,
pamoja na kizazi cha pili, cha tatu na cha nne, kwa damu ya Yesu. Naachilia
baraka za Bwana juu yetu, baraka za kizazi hadi kizazi, baraka za Ibrahimu, na
baraka zote. Katika jina la Yesu.
Baba
katika jina la Yesu. Navaa silaha zote za Mungu, napokea chapeo ya wokovu,
navaa dirii ya haki kifuani, natwaa ngao ya
imani, najifunga kweli kiunoni, nafungiwa miguu yangu utayari niupatao kwa
injili ya amani na upanga wa roho ambao ni neno la Mungu kwa sala zote na maombi nikisali kila wakati katika Roho
kwa mujibu wa Efeso 6: 10-18
Baba
kwa mujibu wa neno lako katika Yer 30:17 Ulisema “Maana
nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana.”
Nakushukuru kwa kutuponya machungu yetu, majeraha, makovu, na maumivu.
Nakushukuru kwa ajili ya kuturejesha tena. Katika Jina la Yesu.
Baba katika Isa 53: 4-5, Ulisema
“Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona."
Bwana nakushukuru kwa neno lako, lina nguvu, linatupatia nguvu, ujasiri,
ulinzi, na uponyaji katika jina la Yesu.
Baba
nakushukuru, kama ulivyosema katika Zaburi 46:1 kwamba wewe ni kimbilio na nguvu,
msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Nakushukuru kwa kuwa tunaweza kukuita
wakati wa shida.
Baba
nasimama sawa sawa na neno lako katika Marko 3:27. Namfunga huyo mtu mwenye
nguvu, nakuvunja kila vizuizi, kamba, vifungo, pingu, minyororo, minyororo ya
utumwa, kutoka katika maisha yangu, wapendwa wangu, na yote yaliyo yangu. Ninaamrisha
mali za mwenye nguvu kuharibiwa, sasa na hata milele. Katika jina la Yesu.
Baba nakushukuru kwa ulinzi wako,
ulisema katika neno lako katika Kutoka 23:27 "
Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote
utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao na
kukimbia. Namshukuru wewe Bwana, kwa nguvu iliyopo katika neno lako
ambayo husababisha maadui kuonyesha maungo yao na kukimbia. Katika jina la
Yesu.
Baba
katika jina la Yesu ninafungua machafuko na upofu wa mungu wa dunia hii, kutoka
kwenye akili zetu, ambazo zinatuzuia kuona mwanga wa injili ya Kristo. Ninaita
kila neno la Mungu linaloingia kwenye akili zetu, na moyo liinuke kwa nguvu
ndani yetu.
Baba wa Mbinguni, asante ninakushukuru
wewe, ninakutukuza wewe, ninakuabudu wewe, nakushukuru kwa neno lako katika
Kumbukumbu 28:7 Bwana atawafanya adui zako wainukao
juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele
yako kwa njia saba. Asante kwa
nguvu yako, ulinzi, na usalama ambao umetoa kwa watoto wako, tukitumia neno,
maadui si tu watakimbia, bali watakimbia kwa njia saba kutoka kwetu, katika
jina la Yesu.
Baba nakushukuru, kwa mikono yako
imara, na mkono wako wa haki wa kulia. Umetuambia, katika 1 Petro 5: 7 Tumtwike yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha
sana na mambo yenu. Bwana nakushukuru kwa kujishughulisha na mambo yetu,
nakushukuru kwa kuwa tayari kwa ajili
yetu wakati tunakuhitaji.
Baba
katika jina la Yesu ninaliadhimisha jina lako; nakupa heshima na utukufu wote
unaotoka kwenye jina lako takatifu. Neno lako linaniambia katika Joshua 1:5 “Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku
zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa
pamoja na wewe; sitakupungukia kamwe wala sitakuacha.” Asante Bwana kwa
ulinzi wako, na baraka.
Baba
nakushukuru kwa neno lako katika 3 Yohana 1:2 linasema kwamba mipango yako kwa
ajili yetu ni ya kutufanikisha, na kuwa na afya njema kama vile roho zetu
zifanikiwavyo. Natumia mamlaka ya neno lako, na kudai ustawi, afya, furaha,
mafanikio, amani ya akili, baraka, na kila mambo mema ambayo umepanga tupate,
juu ya maisha yangu, wapendwa wangu, mali na vitu vyote nilivyonavyo, katika
jina la Yesu.
Baba
wa mbinguni neno lako katika Luke 8:11 linatuambia kwamba neno lako ni mbegu,
na mioyo yetu ni ardhi. Bwana ninakuomba utayarishe mioyo yetu kupokea neno
lako na kulificha katika mioyo yetu, tusitende dhambi dhidi yako, kwa jina la
Yesu.
MAOMBI YA NENO YA UKOMBOZI TOKA KITABU CHA ZABURI
1. Ee Mungu wangu,
uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. Zaburi 59:1
2. Uwakomeshe kwa hasira, Uwakomeshe watoweke, Wajue ya kuwa Mungu
atawala katika Yakobo, Na hata miisho ya dunia. Zaburi 59:13
3. Ee Mungu, uniokoe,
Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu. Zaburi
69:1
4. Uniponye kwa kunitoa
matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika
vilindi vya maji. Zaburi
69:14
5.
Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba
yako. Zaburi 122:7
6. Ubaya wao wasio haki
na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno
Ndiye Mungu aliye mwenye haki.
Zaburi 7:9
7.
Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.
Zaburi 2:9
8. Ee Mungu, usiwe mbali
nami; Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia. Zaburi 71:12
9. Bwana, Mungu wangu,
nimekukimbilia Wewe, Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye. Zaburi 7:1
1. Na jicho langu limewatazama walioniotea, Sikio langu limesikia
habari za waovu walionishambulia. Zaburi 92:11
MAANDIKO YA MAOMBI YA UPONYAJI
1.
Zaburi
91:16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami
nitamwonyesha wokovu wangu.
2.
Zaburi
103:3 Ee nafsi
yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote.
Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa
yako yote
3.
Yeremia
30:17 Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya
jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni
Sayuni, ambao hapana mtu autakaye.
4.
Zaburi
118:17 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia
matendo ya Bwana.
5. Yohana
10:10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu;
mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
6. Zaburi 107:20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo
yao.
MAOMBI YA NENO YA MAJINA YA MUNGU
1. Nalibariki jina lako Yehova -Yire
— "Bwana atatupatia" (Mwanzo 22:13-14)
2. Nalibariki jina lako Yehova -Rafa
— "Bwana uniponyaye" (Kutoka 15:26)
3. Nalibariki jina lako Yehova -Nisi—
" Bwana ni bendera yetu" (Kutoka 17:8-15)
4. Nalibariki jina lako Yehova -Shalom
— "Bwana ni amani yetu" (Waamuzi 6:24)
5. Nalibariki jina lako Yehova -Raah
— "Bwana ni mchungaji wetu" (Zaburi 23:1)
6. Nalibariki jina lako Yehova -Tsidkenu
— "Bwana ni haki yetu" (Yeremia 23:6)
7. Nalibariki jina lako Yehova -Shammah
— " Bwana yupo hapa " (Ezekieli
48:35)
MAOMBI
YA NENO YA KUAMRISHA VIUNGO VYA MWILI WANGU KUFANYA MAPENZI YA MUNGU
1. Ee Bwana, naamuru mikono yangu
kuinuliwa na kumtukuza Bwana kwa jina la Yesu
2. Ee Bwana, naamuru mikono yangu
kubarikiwa, kustawi, na kufanikiwa katika mambo yote yaliyoko katika mapenzi ya
Mungu kwa ajili yangu katika maisha yangu. Katika jina la Yesu.
3. Oh
Bwana, naamuru macho yangu kukutazama wewe, ili kamwe nisipoteze lengo langu.
Katika jina la Yesu.
4. Ee
Bwana, naamuru miguu yangu kutembea
katika njia ya haki, ambapo sitaogopa mabaya kwa jina la Yesu.
5. Ee
Bwana, naamuru masikio yangu kusikiliza mambo mazuri yenye ripoti nzuri.
6. Ee
Bwana, naamuru kinywa changu kuzungumza maagizo ya Mungu, neno la Baraka litoke
kwenye kinywa changu.
7. Ee
Bwana naamuru mawazo yangu kuwafanywa upya kwa neno lako kila siku.
8. Ee
Bwana, naamuru mwili wangu mzima kutolewa kwako, kama dhabihu iliyo hai,
takatifu, na wenye kukubaliwa kwenye huduma yako. Katika jina la Yesu.
MAOMBI
KIMAANDIKO KWA BARAKA NA SHUKURANI
1. Baba katika jina la Yesu
nitashukuru kwa Bwana, kwa maana u mwema, upendo wako, na fadhili zako ni za
milele
2.
Baba
tunaomba utupe nguvu, na utubariki kwa amani katika jina la Yesu Zaburi 29:11
3. Baba
umetuambia kwamba utatuepusha na maovu yote na kuhifadhi maisha yetu. Bwana
utaangalia kutoka kwetu, na kuingia kwetu, tangu sasa na hata milele
4. Bwana nitakushukuru; Nitaliita
jina lako, na kukufanya ujulikane kati ya mataifa kwa yale uliyofanya kwangu
5. Neema ya Bwana wetu
Yesu Kristo na iwe pamoja nasi sote.
2 Thes 3:18
MAOMBI
YA VITA YA KUTUMIA ALAMA ZA MUNGU
Adui
anakuja kuiba, kuua na kuharibu kila kitu chetu, ni lazima kuwa tayari
kupambana na maadui, tujue silaha zetu, na kutumia neno la Mungu. Ni lazima
kujifunza neno la Mungu na kulitumia katika maisha yetu ya kila siku.
Baba neno lako katika Yer 23:29
linasema “Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana;
na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande? ”Nasimama sawa sawa na
neno lako, na kuvunja vipande vipande kila mipango ya kishetani, miradi na kazi
mbaya za adui, katika pepo nne za dunia, katika jina la Yesu.
Baba
neno katika Waebrania 4:12 "linasema “Maana Neno
la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote
ukatao kuwili. Nachukua mamlaka ya neno lako ambalo ni upanga na kugawanya
nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani
ya kila nguvu za uchawi, kila enzi, falme, mamlaka, wakuu wa giza, mapepo
wabaya katika ulimwengu wa roho, mishale ya moto ya adui, maadui wa siri,
maadui wanaojulikana, mapepo ya utambuzi, maadui wa ndani, na mamlaka zingine
zote za adui, kwa kuwafunga na kuwatupa katika shimo milele, katika jina la
Yesu, Amina.
Baba
neno lako katika Yer 23:29 linasema “Je! Neno langu
si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande? ”.
Natumia moto wa Mungu Mwenyezi, kuchoma kila kazi ya adui kama majivu. Chochote
ambacho kilitumwa kwangu, kinachonifuata, kilichohamishiwa kwangu, au kwenye kitu
chochote ambacho ni changu. Nazifunga, na kuzitupa katika lile ziwa la moto,
sasa na hata milele, katika jina la Yesu.
Baba
neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu Zaburi 119: 105.
Nasimama sawa sawa na neno lako, na kutumia mwanga wako kuangaza kila mahali
penye giza ambapo jua haliangazi. Naweka wazi kila matendo mabaya yanayotendeka
kwenye maisha yangu, familia, watoto, fedha za nyumbani, kazi, huduma, ndoa, na
yote ambayo ni yetu. Bwana nakushukuru kwa kufanya kazi za uovu wao kuwa
dhaifu, zife, zifungwe na kufutwa, katika jina la Yesu.
Baba
neno lako katika Yakobo 1:22-25 "linasema kwamba neno lako ni kama
kioo" Natumia mamlaka ya neno lako, na kubamiza, kuangamiza vipande
vipande vioo vyote vya mapepo, ambavyo adui hutumia kufuatilia maendeleo yetu,
mafanikio, baraka, na yote yaliyo yetu. Naamrisha maadui, kuona shughuli zao mbaya,
kushindwa, na anguko katika vioo vyao vya
kipepo, katika jina la Yesu.
Baba
neno lako ni kama maji ambayo yatusafisha dhambi zote na uovu. Waefeso 5:26-27.
Natumia maji ya Bwana Mungu mwenyezi kuwazamisha maadui, mafarao wote,
mayezebeli, goliati na maadui wengine wote wa maendeleo yetu katika bahari
Shamu, sawa sawa na Kutoka sura ya 15
Baba
neno lako linaniambia katika Zaburi 107:20 "Kwamba neno ni kama dawa"
Nasimama sawa sawa na neno lako ambalo ni kama dawa, na kuponya mioyo yetu na
machungu yote, uponyaji wa kimwili, kiakili, kihisia, na kiroho. Naomba neno
lako liturejeshee mara mia moja, kila kitu tulichopoteza, katika jina la Yesu
OMBA
NENO ASUBUHI, MCHANA NA USIKU. OMBA NENO BILA KUKOMA. OMBA MPAKA UKOMBOZI UJE.
Nimeipenda hii
ReplyDeleteAmina
ReplyDeleteAmen
DeleteAmen
Deleteamen
ReplyDeleteAmen. Nimepokea neno.
DeleteAmeen
DeleteUbarikiwe mtumishi, napokeayote niliyoomba. Amen
DeleteMUNGU AKUBARIKI KWA MAFUNDISHO MAZURI
ReplyDeleteUtukufu ni kwa NIKO AMBAYE NIKO
DeleteMungu akubariki sana sana MTU wa Mungu. Hakika nimebariiwa sana. By Renatus 0752234601
DeleteAmen,Amen
ReplyDeleteAmen.
ReplyDeleteameen
ReplyDeleteAmen.
ReplyDeleteAmen.barikiwa sana Mungu azidi kukuinua uendelee kugusa maisha ya wengine
ReplyDeleteBarikiwa mtumishi wa Mungu
ReplyDeleteAmen and Amen
ReplyDeleteAmen!ninazidi kubarikiwa na neno lako,Mungu akubariki muandaaji wa neno hili LA injili takatifu
ReplyDeleteAmen!ninazidi kubarikiwa na neno lako,Mungu akubariki muandaaji wa neno hili LA injili takatifu
ReplyDeleteAsante kwa mafundisho yenye kujengea Imani zetu na kutupa maongozo bora wa namna ya kuomba kwa kudai ahadi za Mungu kwetu. Tukiamini kuwa huwezi kutuahidi halafu asitupe, kumbe basi ni sisi wenyewe tunafanya maisha yetu kuwa magumu kwa kushindwa kuziishi ahadi za Mungu. Barikiwa sana mtumishi.
ReplyDeleteAmina. Mungu akubariki zaidi
ReplyDeleteNashukulu
ReplyDeleteAmen
ReplyDeleteAmen
ReplyDeleteBwana Mungu akuangazie nuru ya uso wake na kukuongeza siku zote za maisha yako. Ubarikiwe sana mtumishi kwa maombi haya uliyotuandalia.
ReplyDelete👏👏🖒
ReplyDeleteFulkotili
ReplyDeleteAmen
ReplyDelete