Luka 2:36 – 37.
Niliwahi kufanya
maombi ya kufunga siku fulani. Kadri ilivyokuwa inasogea jioni nilikuwa nasikia
njaa sana ambapo kuna muda nilataka hata nifungulie kwa kula chochote, lakini
ndani kabisa nilishuhudiwa kuendelea na kukamilisha. Nashukuru Mungu niliweza
kumaliza ule mfungo vizuri, ila ukweli ni kwamba njaa niliyokuwa nayo haikuwa
ya kawaida. Nimeshawahi funga mara nyingi kavu na siku nyingi kuliko hiyo siku
lakini sikuwahi kuona njaa kama safari hii.
Jioni sasa ndiyo
Roho Mtakatifu akanifundisha kwamba kwa jinsi huyu mtu wa nje alivyokuwa
anasikia njaa ndivyo mtu wa ndani anavyosikia njaa ya NENO LA MUNGU
asipolishwa. Taabu ile ile uliyopata kwa mtu wan je ya njaa ndivyo mtu wa ndani
anavyosikia sema tu yeye ni mpole kwa hiyo hadai kwa nguvu kama huyu mtu wa nje
anavyodai chakula na akilishwa anataka kupumzika. Mtu wa ndani akilishwa vizuri
anapokea maagizo toka kwa Mungu na atafanya yale yanayompendeza Mungu.
Tazama jinsi mtu
wa nje alivyowekewa ratiba ya lishe inayozingatiwa kwa umakini:
a.
Kifungua kinywa - Breakfast
b.
Chakula cha mchana - Lunch
c.
Chakula cha jioni - Supper
d.
Chakula cha usiku – Dinner
Tena saa
nyingine anapangiwa maeneo maalumu ya kula nyumbani sebuleni, hotelini,
mgahawani, beach n.k huku mkiongozana na wapendwa wenu. Mtu wa ndani hana
ratiba ya kulishwa wala hana maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili yake, hana
pia mtu wa kungozana naye kwenye kula chakula chake na wakati Roho Mtakatifu
yupo.
Hivi Roho
Mtakatifu ananiuliza ni wangapi wanaojenga nyumba zao wanakumbuka kujenga
chumba maalumu cha kumlisha mtu wa ndani na maombi? Hapa wengi tutaangukia pua
maana wengi wetu nyumba zetu zina vyumba maalumu kama vile study room, maktaba,
sebule ya wageni maalumu, chumba cha mazoezi n.k lakini je kuna mwenye nyumba
iliyojengwa au anayopanga kujenga ina eneo maalumu kwa ajili ya mtu wa ndani?
Kawaida ya
wanadamu wengi tunampenda sana mtu wa nje kwani ana bajeti za kila namna za
kumwezesha kuishi kwa raha, mifano japo michache:
a.
Chakula
b.
Vinywaji
c.
Burudani
d.
Likizo
e.
Sherehe
f.
Mavazi
g.
Malazi
h.
Elimu n.k.
Mtu wa ndani je
naye hastahili kuwa na bajeti yake? Mifano michache tu:
a.
Biblia
b.
Ibada za Jumapili na nyinginezo
katika wiki
c.
Vitabu vya watumishi waliopakwa
mafuta na Bwana
d.
Semina
e.
Mikutano ya injili
f.
Warsha za injili
g.
Mikesha
h.
Elimu n.k
Tujiulize kati
ya mtu wa ndani na wa nje ni yupi ambaye anapata mahitaji karibia yote japo
nimetaja machache.
Wapendwa mtu wa
ndani anaathirika sawa sawa na mtu wa nje anapokosa chakula. Kama mtu wa nje
akikosa chakula anapata utapiamlo, magonjwa, udhaifu na mtu wa ndani pia
anapata utapiamlo, magonjwa, udhaifu n.k.
Ni bora mtu wa
ndani apate chakula chake kuliko wa nje maana sisi halisi ni mtu wa ndani wala
sio wa nje. Mtu wa ndani akiwa vizuri wa nje naye lazima atakuwa vizuri.
Mungu akupe
maarifa na ufunuo wa kumlisha na kumtunza mtu wa ndani katika jina la Yesu.
Amen, nawe barikiwa kwa kusoma.
ReplyDelete