Thursday, March 3

NIANZIE WAPI?

 


Je hujui mahali pa kuanzia ili jambo unalolipanga lilete mafanikio kwako?

Inaweza kuwa hujui uanzie wapi kuhusu huduma, ndoa, biashara, kilimo, ufugaji, elimu, kutatua changamoto Fulani ya kimaisha na kadhalika, orodha inaweza kuwa ndefu sana. 

Kama hujui basi usiogope tulia suluhisho lipo hapa, kuna mambo manne muhimu ya kufanya ili mambo yaende vizuri.

 

1.    Maombi 


Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

 

Hatua ya kwanza kabisa ni kumjulisha Mungu hiyo haja yako kwa njia ya

Maombi. Acha kujisumbua kwa mawazo mengi yasiyokuwa na majibu, maana ukijisumbua neno la Mungu linasema kwenye Matayo “Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?”. Rafiki tulia kwanza mwendee Baba yako wa mbinguni kwenye chumba chako cha siri, neno lake linasema ukiwa hapa sirini yeye anakuona na atakujazi (Matayo 6:6)

 

Bwana Yesu anatuhakikishia amani, ghafla ukiwa chumba cha siri unaona unapata amani ya ajabu, kufadhaika na hofu ulizokuwa nazo kuhusu hilo jambo lako vinatoweka ghafla kwa sabubu (Yohana 14:27). Sasa unapokuwa na amani ya Kristo utaona unaweza kufanya maamuzi sahihi kwa sababu amani ya Kristo moyoni mwako ndiyo inaaza kukuwezesha kuamua, utanza kupata mwelekeo wa kile unachotaka kufanya.

 

Ukiwa chumba cha sirini utaaza kuona ukaribu wa Mungu na kuu wake maana umemwita na umemfanya wa kwanza kwenye mipango yako kwani neno lake linasema kwenye Zaburi ukimwita anakuwa karibu na wewe.

 

Zaburi 145: BWANA yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.


 

2.      Tafuta ushauri

 

Mithali 15:22 Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.

 

Msatri wetu hapu juu unatusisitiza umuhimu wa kupata ushauri kwa sababu pasipo ushauri wa kutosha makusudi ya mipango yetu ni vigumu kufanikiwa, lakini tukipata ushauri wa kutosha na sahihi makusudi ya mipango yetu yatafanikiwa.

 

Jitahidi kutafuta ushauri toka kwa watu waaminifu ambao hawatateka nyara wazo lako.Unaweza omba ushauri toka kwa viongozi wako wa kiroho, washauri wa bobezi wa hilo jambo lako, watu waliokutangulia kufanya unachotaka kufanya, makampuni ya ushauri waliosajiliwa na mamlaka za nchi.

 

Ukishapata ushauri wa kutosha anza kuchambua ushauri ulio bora ili uweze kuufanyia kazi, muda mwingine unaweza kuta kuna vipengele mbalimbali tofauti toka kwa washauri mbalimbali ambavyo inakubidi kuviunganisha ili kupata kitu kilicho bora, kwa hiyo sio vibaya kuchanganya ushauri A na B kupata kitu kilicho bora.

 

 

3.      Utafiti

Mithali 19:2 Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

Hatua inayofuata ni kutoka sasa ndani na kwenda kufanya utafiti wa kile unataka kufanya, mstari wetu hapo unazungumzia maarifa. Unapfanya utafiti wa kitu unaazna kupata maarifa ya kile unaenda kufanya, kwenye utafiti utapata taarifa mbalimbali zinazoweza kukupa maarifa. 

Mfano unataka kuingia kwenye kilimo ni lazima ufanye utafiti wa maeneo bora kwa kilimo kwa kujua hali ya hewa, aina ya udongo, mazao yanayostawi hilo eneo, usafiri wa uhakika, aina za mbolea, muda wa kupanda, kupalilia, kuvuna, masoko ya kuuza mazao yako, bei za sokoni zipoje.

Je unataka kulima mazao ya aina gani ya muda mrefu au mfupi, mazao ya biashara au chakula, mazao yako ni ya kuuza ndani au nje ya nchi. Kwa hiyo taarifa zote za utafiti huu zitakusaidia kupata maarifa sahihi ya kuanza kufanya kilimo.

Neno la Mungu linasema kwenye kitabu cha Hosea 4:6 kwamba ‘watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”. Na ili kupata maarifa lazima kufanya utafiti kwa kusoma vitabu, kujifunza kwa waliokutanglia tena wale waliofanikiwa, kwenda eneo la tukio na kujifunza mazingira yake.

 

4.      Tengeneza mpango wa biashara (Business plan)

 

Mithali 24:27 Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako.


Proverbs 24:27 (NLT) "Do your planning and prepare your fields before building your house.” 

Nimeweka huo mstari kwa lugha ya kingereza ili kurahisisha uelewa  maana kwenye Kiswahili pana ugumu kidogo wa kuelewa.

Mpango ni kitu muhimu sana kwenye maisha ya kila siku, sasa kuna hichi kitu kinaitwa mpango wa biashara huu mpango sio kwenye sekta ya biasha tu ndiyo unatakiwa uwepo, kimsingi kwenye kila eneo la maisha huu mpango unatakiwa uwepo au upo lakini unaweza kuwa na jina tofauti kidogo.

Kuna mahali Yesu anasema ukitaka kujenga mnara lazima ukae chini ufanye mahesubu kwanza kama unaweza kuumaliza au la.

Luka 14:28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? 29Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, 30wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza

Ni muhimu kuwa na mpango wa biashara ambao utakuwezesha kufanya jambo lako hatua kwa hatua mpaka utakapoona mafanikio. Kama hujui jinsi ya kuanda mpango wa biashara kuna watu au makampuni ambayo unaweza kwenda kwao na wakakupa hiyo huduma kwa gharama nafuu sana.

Naamini kwamba kwa sasa umepata mwanga wa mahali kwa kuanzia, maana ukimshirikisha Mungu ambaye ndiye chanzo hata la wazo la mpango wako, yeye huwa ana kawaida ya kutimiliza kile alichkiaanzisha moyoni mwako.

Wafilipi 1:6 Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;Mungu mwenyewe ndiye anayefanya kazi ndani yetu ili kutimiza kusudi lake jema.Wafilipi 2:13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.

 

 

 


No comments:

Post a Comment

Barikiwa kwa ujumbe wako.