Warumi 8:1
Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
Hata wakati mbaya kabisa wa giza katika historia, Mungu alikuwa kazini, ili kuhakikisha mwanadamu anapata wokovu.
Pale Msalabani palikuwa na mabadilishano ya Kiungu ambapo hukumu ya kifo tuliyostahili ilibadilishwa kwa rehema yake na tukapewa uzima wa milele.
Hii ndiyo sababu tunasheherekea Ufufuo wa Yesu Kristo.
Alikamatwa
Aliteswa
Alipigwa
Alidharauliwa
Alivuliwa nguo zote
Alidhalilishwa
Alisemwa vibaya
Alipingwa
Alihukumiwa pasipo kosa
Alitemewa mate
Alichekwa
Alifanyiwa ukatili wa kutisha
Alifyonywa
Alitikisiwa kichwa
Alikodolewa macho
Alizuiliwa mikono na miguu
Aliharibiwa
Alisulubiwa pamoja na wanyang'anyi
Alichomwa mkuki ubavuni
Alisema Mungu wangu mbona umeniacha
Hakuweza tena kumwita Mungu, BABA kama alivyozoea
Kwa sababu alifanyika dhambi ili sisi tuhesabiwe haki
ALISEMA IMEKWISHA
Alimkabidhi Mungu Roho yake
Alizikwa kaburini
Alifungiwa na jiwe kubwa lenye muhuri
Alilindwa kuhakikisha hafufuki
Alishuka kuzimu
SIKU YA TATU AKAFUFUKA TOKA KWA WAFU
Jiwe halikumzuia kutoka kaburini
Yote hayo yalifanyika ili mimi na wewe tupate uzima wa milele
Ndugu unayesoma ujumbe huu wa Pasaka njema ya Ufufuo, kama hujampa Yesu maisha yako, basi nakuomba useme maneno haya hapa chini ili ufanyike Mwana wa Mungu.
Mungu wangu ninamkiri Yesu kwa kinywa changu ya kuwa ni Bwana, na ninaamini moyoni mwangu ya kuwa wewe Mungu ulimfufua katika wafu, kwa hiyo nimeokoka.
Kwa maana kwa moyo nimeamini hata kupata haki, na kwa kinywa nimekiri hata kupata wokovu.
Asante Yesu kwa Neema yako.
Asante Mungu kwa pendo lako.
Asante Roho Mtakatifu kwa ushirika wako.
Basi ndugu mpendwa umekuwa mwana wa Mungu, hongera sana kwa muujiza huu mkubwa kabisa wa kuokoka.
Yohana 1:12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
Ukiwa unahitaji msaada wa jinsi ya kukua kiroho tuwasiliane kwa namba hii 0754809462.
Frank Riessen
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
-
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na ...
-
I. OMBEA KANISA LAKO A. Omba mara kwa mara kwa ajili ya Kanisa – Kuombea Kanisa mara kwa mara itasaidia mioyo yetu kujiunganisha na...
-
Watu wengi wanaamini kwamba Mungu anaweza kuwaponya lakini hawana uhakika kama atawaponya wao. Kama huyo ni wewe, basi nakutia moyo usome k...
No comments:
Post a Comment
Barikiwa kwa ujumbe wako.