Luka 7:12,14-15
12 Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye.
14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka.
15 Yule maiti akainuka, akaketi, akaanza kusema. Akampa mama yake.
Pengine ni ndoa, huduma, biashara, mtoto, kazi yako ipo langoni kwa mji inaenda kuzikwa (Na ya pekee kabisa)
Usiogope maana Yesu mtoa UZIMA anakutana na huo msafara wa mauti unaokwenda kuzika maono yako.
Yesu anaiambia ndoa, huduma, biashara, elimu, kazi, mtoto wako aliyeshindikana INUKA NAKWAMBIA nayo bila kusita inainuka na Yesu anakukabidhi upya kile kilichokuwa kimekufa.
UZIMA ukikutana na mauti, mauti haiwezi kuhimili itakimbia tu.
Baki umebarikiwa mwana wa Mungu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
-
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na ...
-
I. OMBEA KANISA LAKO A. Omba mara kwa mara kwa ajili ya Kanisa – Kuombea Kanisa mara kwa mara itasaidia mioyo yetu kujiunganisha na...
-
Watu wengi wanaamini kwamba Mungu anaweza kuwaponya lakini hawana uhakika kama atawaponya wao. Kama huyo ni wewe, basi nakutia moyo usome k...
No comments:
Post a Comment
Barikiwa kwa ujumbe wako.