Friday, January 24
VINASABA (DNA) YAKO NI VYA NANI?
Baada ya anguko Adam hakuweza kuzaa mtu kwa sura na mfano wa Mungu.
Ndiyo tunasema dhambi ya asili, kwa sababu tuna VINASABA (DNA) vya Adamu
Mwanzo 5:3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.
Tunahitaji kuzaliwa na Mungu ili tuwe na VINASABA (DNA) vya Mungu.
Ili uzaliwe kwa sura na mfano wa Mungu una jukumu la kumpokea Yesu kwenye maisha yako.
Yohana 1:12-13 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; 13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.
Tena neon la Mungu linatuambia tunazaliwa kwa mbegu isiyoharibika.
1 Petro 1:23 Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.
Sasa tuna VINASABA (DNA) vya BABA yetu wa Mbinguni
Kama tu wana wa Mungu kinachotokea ni hichi hapa chini:
1 Yohana 3:2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
-
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na ...
-
I. OMBEA KANISA LAKO A. Omba mara kwa mara kwa ajili ya Kanisa – Kuombea Kanisa mara kwa mara itasaidia mioyo yetu kujiunganisha na...
-
Watu wengi wanaamini kwamba Mungu anaweza kuwaponya lakini hawana uhakika kama atawaponya wao. Kama huyo ni wewe, basi nakutia moyo usome k...
No comments:
Post a Comment
Barikiwa kwa ujumbe wako.