"Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na
kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi
lake" (Warumi 8:28).
Keki ni tamu lakini utamu huo umepatikana baada ya kuchanganya
vitu ambavyo ukivila vyenywe hupati ile ladha ya keki.
Kwa mfano,
chumvi, mayai, sukari, unga ngano, baking soda n.k. Hivi vitu ukila hivi hivi
kimoja kimoja hupati ladha nzuri ya keki, lakini vikichanganywa kitaalamu kwa
uwiano maalumu na kupikwa unapata keki yenye ladha nzuri sana, ambayo ni
tofauti sana na ladha ya kila kimoja kati ya viungo vyake.
Ndivyo
na Mungu wetu alivyo, anatumia vitu vyote vizuri na vibaya kukupata mema.
Hayo
mabaya na mazuri Mungu anayatumia kukupatia mema, sawa sawa na Warumi 8:28.
Angalia
pia Ayubu alijua siri hii tangu zamani,
"9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe. 10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake" (Ayubu 2:9, 10).
"9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe. 10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake" (Ayubu 2:9, 10).
Usije
ukaanza KUMCHUKIA Mungu wakati anaweka pilipili na chumvi maishani mwako, hapo
ndio ANAKUTENGENEZA uwe kitu BORA zaidi.
Frank
P. Seth & Frank R. Makundi
No comments:
Post a Comment
Barikiwa kwa ujumbe wako.