Zaburi 138:8 Bwana
atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi
za mikono yako.
Hakika Mungu anatutea
katika mambo yetu, kuna haja nyingi sana ambazo tunazo lakini kumbe
tukimshirikisha/tukimtegemea Mungu huwa anatimiliza mambo yetu.
Na kwa sababu fadhili
zake ni za milele, kamwe hatatuacha kama alivyoahidi kwamba; na tazama, mimi nipo
pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari, Mat 28:20b.
Sisi ni kazi ya mikono
yake, tukimwita kwa kumaanisha kama Bartimayo,
atatusikia maana nguvu ya Mungu siku zote huwa inasikilizia kilio cha imani,
halafu inatenda kazi katika ile imani. Ndipo Yesu husema; Enenda zako, imani
yako imekuponya, Mak 10:52. Lakini je tupo tayari baada ya kuisikia hii sauti
ya Yesu ya Enenda zako, imani yako imekuponya?
© Frank R.M Makundi.
No comments:
Post a Comment
Barikiwa kwa ujumbe wako.