Wednesday, July 1

UFALME WA MUNGU/MBINGUNI SEHEMU YA KWANZA

Naona kuna vitu viwili tunashindwa kutofautisha katika haya mambo tunayojadili/changia, vitu hivyo ni
1.      Dini iliyoasisiwa na mtu kumtafuta Mungu
2.      Ufalme wa Mungu/Mbinguni uliorejeshwa na Yesu kumrejesha mtu kwa Mungu (Wokovu).

DINI ILIYOASISIWA NA MTU KUMTAFUTA MUNGU
Dini inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji.

Kwa misingi hiyo tunaona kwamba dini zote zinafanana katika malengo yao ya kumtafuta Mungu. Kwa hiyo kwa ujumla Dini ni mpango wa mtu kumtafuta Mungu. Sasa basi katika huu mpango wa mtu wa kumtafuta Mungu kunakuwa na namna tofauti tofauti za kumfikia huyo Mungu na zote kwa mtazamo wa mtu ni sahihi hazina shida.

Dini ni matokeo ya njaa ya roho ya mwanadamu ambayo mtu bado hajaweza kuifafanua ila bado anatafuta ili ajiridhishe njaa yake ya rohoni (satisfaction). Njaa hii isiyokuwa na ufafanuzi inasababishwa na uwazi uliobaki baada kitu fulani kupotea toka kwa mtu ambacho alikuwa anakimiliki.
Mtu  baada ya kuasi na kuupoteza utaratibu wa ibada uliowekwa na Mungu pale Eden alianza kutafuta njia ya kuupata uwepo wa Mungu.
Maana mtu kwa jinsi alivyoumbwa hawezi kukaa nje ya uwepo wa Mungu, ni kama samaki ukimtoa kwenye maji atakuwa na machaguo mawili kufa au kutafuta njia ya kurejea kwenye maji ambayo ndo maisha yake (uzima wake) upo. Kwa hiyo na mtu kama samaki ni lazima akae kwenye uwepo wa Mungu/Eden.
Sasa basi huyu mtu akaanza kuitafuta Eden/uwepo wa Mungu, ndiyo tunaona dini zinaanzishwa, dini zinagawanyika katika madhehebu n.k hii yote ni kuitafuta Eden/uwepo wa Mungu.
Lakini ukiangalia madhumuni ya dini zote yanafanana mfano wa mambo machache ni 1)dini zote zinadai kwamba ni za kweli 2)zinadai zinamwamini Mungu 3) zinadai Mungu ni mmoja 4) zinadai zina haki 5) zinadai zinaweza kutoa amani na utulivu 6) zinadai zinaweza kutoa uwezo na nguvu 7) zinadai zenyewe ni bora kuliko nyingine n.k.
Shida ya dini zote badala ya kumuunganisha mwanadamu kwa nguvu na maarifa ya pamoja, dini zimekuwa mgawanyaji mkuu wa wanadamu.
Dini zote zinautaratibu wa kuendesha imani zao na zinatofautiana toka dini moja kwenda dini nyingine kadhalika na madhehebu ya hizo dini. Na taratibu zote zina lengo la kufikia kile kilichopotezwa kwenye bustani ya Eden.
Baadhi ya taratibu ni vitu kama liturujia, madhabahu, mapokeo, jinsi ya kuwa mshirika wa hizo dini mfano ubatizo, kusilimisha, kujaza fomu maalumu, kuunganishwa kwa njia ya kutaja majina ya wanaukoo wote, viapo na nadhiri mbalimbali.
Lengo la yote hayo ni kutafuta kilichopotea bustani ya Eden (uwepo wa Mungu) ili mtu aweze kuishi.
DARAJA KUELEKEA UFALME WA MUNGU/MBINGUNI ULIOREJESHWA NA YESU KUMREJESHA MTU KWA MUNGU (WOKOVU)
Tukibaki kwenye dini ni lazima mabishano, majigambo, kiburi, sifa, kujiona mwenye haki zaidi ya dini nyingine kutatokea, lakini tukijadili kwa kufuata kusudi kuu la Mungu mambo yatakwenda vizuri na hatimaye Mungu atatukuzwa.
Ukristo (Christianity) kwa wanaofuata mpango wa Mungu wa Mwanzo 3:15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.
Ukristo sio DINI.UKRISTO ni uzima wa Mungu ndani ya Mtu, ni mfumo kamili wa wa maisha yenye uzima wa Mungu ndani ya Mtu.
Kusudi kuu la Mungu linapatikana kwenye Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Kwa hiyo dhumuni/kusudi kuu la Mungu kumuumba mtu ni ili KUTAWALA maana nyingine ni UFALME (sovereign rule). Na hii ni kwa sababu Mungu alitaka kuongeza utawala wake usioonekana uje kwa jinsi ya kuonekana kwa njia ya mwanadamu, kwa hiyo Mungu anataka kushirikiana na sisi katika kutawala.

Tunachotakiwa kufanya ni kuifanya hii dunia kuwa koloni la Mbinguni, mbinguni hakuna ujima, ukabaila, ubepari, ubeberu, ujamaa, demokrasia. Mbinguni lugha ya utawala inayoeleweka ni Mfalme na Ufalme na Wafalme. Wafalme wanatajwa hapa ni wote walioukubali huu mpango wa Mungu kwenye Mwanzo 3:15.

Kwenye Mwanzo 3 kuna habari ya anguko la mwanadamu hapo ndiyo mwanzo wa kuchanganyikiwa kwa wanaadamu katika mahusiano yao na Mungu. Lakini pia tunaona Mungu akitangaza mpango wa kurejesha alichokipoteza Adam, Mwanzo 3:15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.

UFALME WA MUNGU/MBINGUNI ULIOREJESHWA NA YESU KUMREJESHA MTU KWA MUNGU (WOKOVU)

Ufalme wa Mungu/mbinguni ni: Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu Rum 14:17

Pale bustani ya Eden mtu alipoteza UFALME hakupoteza DINI, hili ni jambo la msingi sana la kukumbukwa na kuelewa. Isaya 9:6 Inasema:  Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.
Unaona huo unabii Isaya anautoa katika wakati uliotimilika, kimsingi Isaya alikuwa anathibitisha kile Mungu alichokisema pale bustani ya Eden, Mwanzo 3:15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.
Tunaelewa kwamba Yesu Kristo ni kichwa cha Kanisa, kwa maana hiyo sisi ni mwili ambao una mabega, kwa hiyo kwa lugha rahisi uweza wa KIFALME tunaoambiwa na Isaya umerejeshwa kwetu. Atukuzwe Mungu maana ahadi zake siku zote ni za kweli na neno lake, litokalo katika kinywa mwake; halitamrudia bure, bali litatimiza mapenzi yake, nalo litafanikiwa katika mambo yale aliyolituma Isaya 55:11.

Angalia Yohana anavyoanza mahubiri yake Matayo 3:1-2 Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.

Kwa sababu neno la Mungu halipingani, linatakiwa kuthibitishwa na mashahidi wasiopungua wawili Yesu naye anaanza kazi yake kwa kukubaliana na Yohana Mbatizaji, Mathayo 4:17 Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.
Kipaumbele kikubwa cha Yesu ni kurejesha UFALME wa Mungu/Mbinguni kwa wanadamu, hebu tuangalie mistari mbalimbali toka Injili kama ilivyoandikwa na Matayo, injili nyingine Luka na Marko zimezungumzia pia ufalme wa mbinguni kwa uchache na Matayo pia ametumia Ufalme wa Mungu kwa uchache lakini mimi nimependa kumtumia Matayo.
Mathayo 3:2 Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.
Mathayo 4:17 Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.

Mathayo 5:3 Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Mathayo 5:10 Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Mathayo 5:19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 5:20 Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 6:9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

Mathayo 7:21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 8:11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;

Mathayo 10:7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.

Mathayo 11:11 Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.

Mathayo 11:12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

Mathayo 13:11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa.

Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

Mathayo 13:31 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;

Mathayo 13:33 Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia.

Mathayo 13:44 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile.

Mathayo 13:45 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri;

Mathayo 13:47 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

Mathayo 13:52 Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.

Mathayo 16:19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.

Mathayo 18:2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

Mathayo 18:3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 18:4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 18:23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

Mathayo 19:12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.

Mathayo 19:14 Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao.

Mathayo 19:23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 20:1 Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.

Mathayo 22:2 Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.

Mathayo 23:13 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.

Mathayo 25:1 Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
Yesu Kristo alisisitiza sana habari ya UFALME kwa sababu ndicho ambacho mwanadamu alikuwa amepoteza na mwanadamu alikuwa katika harakati mbalimbali za kurejesha kilichopotea tunaona kulikuwa na madhehebu mbalimbali kama vile Masadukayo, Mafarisayo n.k, na wote hawa walikuwa wanatofautiana katika kurejesha kile kile walichopoteza na walipingana kweli kweli na pia walimpinga na kumpa Yesu changamoto mbalimbali ili kuonyesha wao ni bora zaidi.
Haya madhehebu hayakuweza kushibisha kiu ya mwanadamu ya kurejesha kilichopotea, kwa hiyo Mungu akakirejesha kwa kupitia mwanae mpendwa.








                                                   





No comments:

Post a Comment

Barikiwa kwa ujumbe wako.