Zaburi 119:18 Unifumbue macho yangu niyatazame
Maajabu yatokayo katika sheria yako.
Sheria ya Mungu ni mfumo
wa kanuni, ambazo zimetolewa na Mungu mwenyewe ili kuratibu mahusiano baina
yake na mwanadamu. Pia ni mkataba ambao Mungu ameundaa ili kumwongoza mwanadamu
kupata ufalme wa mbinguni.
Katika
sheria ya Mungu mwanadamu hajashiriki katika kuitunga hii sheria, anachotakiwa
mwanadamu ni kuifuata kama ilivyo, maana Mungu ni upendo kwa hiyo sheria yake
ni ya upendo.
Kwenye
ufalme hamna demokrasia, ujamaa, ubepari, ujima, ukabaila wala mfumo wowote wa
utawala unaoujua zaidi ya sheria ya KIFALME. Neno la Mfalme ni sheria ndiyo
kusema neno la Mungu ni sheria na kitu cha ajabu kabisa Mungu mwenyewe hawezi
kuwa juu ya neno lake. Hujanielewa nasema Mungu mwenyewe yupo chini ya Neno
lake, Zaburi 89: 34
Mimi sitalihalifu agano langu,
Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu. Maana yake kama hawezi
kuliahalifu wala kulibadili neno linalotoka kinywani mwake kwa hiyo yupo chini
ya neno lake.
Ukiangalia sheria za
kidemokrasia zinaanza kwa kusema ‘Sisi tumeamua hivi’ lakini sheria ya Mungu
inasema ‘Mungu akasema’ ‘Mimi ni’ ‘Nime’. Kwa hiyo hapa hamna demokrasia ni
sheria tu. Lakini ni sheria ambazo tukizifuata zinatuwezesha kula mema ya nchi
na hatimaye uzima wa milele. Mungu pia ametushauri tuchague uzima, katika Kumbukumbu la Torati 30:19 Nazishuhudiza
mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti,
baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;
Msatari
wetu wa ufunguzi una ombi kwa Mungu kwamba atufumbue macho yetu tuyaone maajabu
yatokayo katika sheria yake.
Kumbe
sheria ya Mungu ina maajabu, kwa hiyo tunatakiwa kumwomba Mungu atufumbue macho
yetu tuyaone hayo maajabu. Yeremia 33:3
inasema: Niite, nami nitakuitikia, nami
nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Bila kumwita/kumwomba Mungu
hatuwezi kuona maajabu ya sheria yake.
Macho
yetu yanahitaji kufumbuliwa ili kuweza kuona, mfano usipojua jinsi ya kumtii
Mungu hutaweza kumpinga shetani, kwa hiyo inabidi kufumbuliwa macho ili uweze
kujua jinsi ya kumtii Mungu ili uweze kumpinga shetani.
©
Frank R.M Makundi
No comments:
Post a Comment
Barikiwa kwa ujumbe wako.